Historia ya Tanzania Historia ya Tanzania inahusu eneo la Afrika Mashariki ambalo wakazi wake leo wanaunda Jamhuri ya Muun...
Historia ya Tanzania
Historia ya Tanzania inahusu eneo laAfrika Mashariki ambalo wakazi wake leo wanaunda Jamhuri ya Muunganowa Tanzania.
Historia ya awali
Nchi ina mabaki ya kale sana yazamadamu (kiumbe aliyekaribiana nabinadamu kwa umbile). Sehemu yaBonde la Ufa, kama Bonde la Oltupai(zamani Olduvai Gorge) lililoko ndani yahifadhi ya Serengeti, ndiko kulikogunduliwa masalia ya viumbe wa jamii ya watu wa kale yenye umrimkubwa kuliko yote yanayojulikana duniani hadi hivi sasa.
Kutokana na ugunduzi huo,wanasayansi duniani wanaamini kuwa Tanzania bara ni chimbuko la binadamu. Ushahidi wa kisayansi unatokana na nyayo za zamadamu zilizogunduliwa katika eneo la Laetolilililoko kusini kidogo mwa Oltupai, umeongeza uzito wa hoja ya Tanzania kuwa chimbuko la binadamu.
Binadamu wa kwanza kuishi huko huaminiwa kuwa wawindaji wa jamii yaWasani, halafu Wabilikimo.
Milenia za mwisho Kabla ya Kristowalihamia huko Wakushi kutokakaskazini, nao wakameza kwa kiasi kikubwa wakazi asili, wakaingiza kilimo,ufugaji na uzalishaji kwa jumla.
Katika karne za kwanza BK walifika kwa awamu kutoka magharibi wahamiajiWabantu wenye ujuzi wa kilimo nauhunzi. Nao wakameza kwa kiasi kikubwa wakazi waliotangulia.
Hatimaye Waniloti kutoka kaskazini walizidi kuingia hadi karne ya 18.
Kanda la pwani pamoja na njia za misafara kuelekea Ziwa Tanganyikavilikuwa chini ya athira ya Usultani wa Zanzibar.
Usultani wa Zanzibar
Eneo la Usultani wa Zanzibar mnamo 1885
Ilianzishwa wakati wa kugawa Usultaniwa Omani mwaka 1856 ikaishia mwaka1964 baada ya mapinduzi ya Zanzibarna muungano na Tanganyika uliozaaTanzania.
Sayyi Said kuhamia Unguja
Usultani ulianzishwa wakati SultaniSayyid Said alipoamua kuhamishamakao makuu yake kutoka Maskat(Omani) kwenda Unguja.
Sayyid Said alikuwa Sultani wa Omani tangu mwaka 1804. Aliimarisha utawalawa Omani juu ya pwani ya Afrika ya Mashariki.
Mwaka 1829 alifaulu kuteka Mombasailiyokuwa mji pekee wa kujitegemea kati ya miji yote ya Uswahilini.
Visiwa vya Unguja na Pemba vilikuwa chini ya Omani tangu mwaka 1689,Wareno walipofukuzwa katika pwani za Uswahilini.
Biashara ya karafuu na watumwa
Sayyid Said aliona nafasi kubwa yabiashara ya karafuu kwa ajili ya soko laUhindi na kwingineko. Mwaka 1829akaanzisha mashamba ya mikarafuu kwa kutumia kazi ya watumwa kutokabara.
Biashara hiyo ikabadilisha uso wa mji wa Zanzibar wa karne ya 19 uliowahi kuwa kijiji kikubwa tu cha vibandakando ya boma lililojengwa na Omani kama kizuizi dhidi ya Wareno.
Baada ya azimio la mwaka 1832 la kuhamisha mji mkuu wa Omani kwenda Unguja, idadi ya wakazi wa mji ilikua haraka.
Nchi za nje zikatambua mji mkuu mpya na kujenga uhusiano. Ubalozi waMarekani ulijengwa mwaka 1837, Uingereza ukafuata mwaka 1841 naUfaransa mwaka 1844.
Sultani mwenyewe aliondoka kabisa Maskat mwaka 1840. Kukua kwa Zanzibar kulisababisha kukonda kwa mji wa Maskat
Bendera ya Usultani wa Zanzibar
Kugawiwa kwa Omani kulikuwa mwanzo wa Zanzibar
Baada ya kifo cha Sayyid Sultan mwaka1856, usultani wa Oman uligawiwa kati ya wanawe. Sayyid Majid bin Said Al-Busaid (1834/1835–1870) akawa Sultani wa kwanza wa Zanzibar na kakayake Sayyid Thuwaini bin Said al-Saidakawa Sultani wa Oman akitawala nchi hiyo bila maeneo ya Afrika ya Mashariki.
Usultani mpya ulikuwa nchi yenye nguvu kati ya Rasi Delgado (mpakani nakoloni la Kireno ya Msumbiji) hadiMogadishu (Somalia). Athira yake ilienea kupitia njia za misafara yapembe za ndovu na watumwa hadi mto Kongo.
Wafanyabiashara kama Tippu Tipwaliokuwa raia wa Usultani wakapitaTabora na Ujiji kwenda ziwa Tanganyikana kuingia ndani ya eneo la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ya leo.Wapagazi wao walibeba bidhaa kutoka Zanzibar zilizobadilishwa kwa pembe za ndovu hasa. Watumwa walikamatwa au kununuliwa wakabeba pembe hadi pwani.
Jumba la Sultani Zanzibar
Sayyid Bargash
Sultani wa pili wa Zanzibar yenyewe, Sayyid Bargash, alijitahidi kujenga uhusiano na nchi za nje. Alifunga soko la watumwa Zanzibar mjini kulingana na mapatano ya kimataifa, lakini akavumilia biashara ya watumwa kuendelea chinichini. Wakati wa Bargash majengo mengi ya Mji Mkongwe yakajengwa.
Mwishowe mwa utawala wake aliona kupungukiwa kwa eneo lake kutokana na mashindano ya nchi za Ulaya ya kuenea katika Afrika baada ya mkutano wa Berlin.
Mwaka 1885 Karl Peters alifanya mikataba ya ulinzi na watawala wadogo waliokuwa chini ya Sultani barani Tanganyika. Upingamizi wa Sultani ulishindikana kwa sababu Wajerumaniwalituma manowari Unguja akapaswa kukubali maeneo mapya ya Wajerumani.
Kuenea kwa ukoloni
Mwaka 1886 mkataba kati ya Uingereza na Ujerumani ulibana eneo la sultani barani katika kanda yenye upana wamaili kumi tu kati ya Rasi Delgado na Mogadishu. Bargash na mfuasi wake Khalifa bin Said waliamua kuuza maeneo hayo au kuyakodisha.
- Pwani ya Tanganyika ikakodishwa kwa Wajerumani mwaka 1888 na hatimaye kuuzwa mwaka 1890.
Waingereza walikuwa walisita kuhusu Zanzibar lakini baada ya jaribio la Karl Peters la kufanya mkataba na Sultani ili kuingiza visiwa hivyo katika Afrika ya Mashariki ya Kijerumani, Uingereza uliamua kutafuta utawala wa visiwa.
Mkataba wa Zanzibar-Heligoland na mwisho wa uhuru
Mkataba wa Zanzibar-Helgoland kati ya Ujerumani na Uingereza ulileta patano la kuwa Zanzibar itakuwa chini ya Uingereza.
Tangu mwaka 1913 nafasi ilichukuliwa na afisa mkazi mkuu.
Kwa muda wa miaka 26 usultani ulikuwa na fedha yake ya pekee iliyoitwa Riali ya Zanzibar.
Koloni la Kijerumani
Maeneo yaliyoitwa baadaye (1920) "Tanganyika" na baadaye tena Tanzania Bara yaliunganishwa mara ya kwanza tangu mwaka 1886 kama koloni laUjerumani lililoitwa Afrika ya Mashariki ya Kijerumani.
Tangu mwaka 1885 Karl Peters, kwa niaba ya Shirika la Ukoloni wa Kijerumani (Gesellschaft für Deutsche Kolonisation) alianza kufanya mikataba na watawala wenyeji katika maeneo yaUsagara, Nguru, Useguha na Ukamiiliyoweka msingi wa madai yake ya kuchukua utawala mkuu wa maeneo hayo.
Uenezeaji wa Wajerumani uliendelea hasa baada ya kushinda upinzani katikavita ya Abushiri na vita dhidi ya Wahehe.
Koloni lile la Kijerumani lilikuwa kubwa kuliko Tanganyika ya baadaye, maana ilijumlisha pia maeneo ya Rwanda naBurundi pamoja na sehemu ndogo yaMsumbiji.
Wakati wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia(1914 - 1918) koloni hilo la Kijerumani lilitekwa na majeshi ya Uingereza naUbelgiji.
Mkataba wa Versailles wa mwaka 1919 ulikuwa na kanuni za kuchukua makoloni yote ya Ujerumani na kuzikabidhi kwa mataifa washindi wa vita. Sehemu kubwa ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani iliwekwa chini ya utawala wa Uingereza, kasoro maeneo ya Rwanda na Burundiyaliyokabidhiwa mikononi mwa Ubelgiji.
Tanganyika Territory ya Kiingereza baada ya kuondoka kwa Wajerumani
Utawala wa Wajerumani ulikoma katika eneo la Tanzania Bara baada ya Ujerumani kushindwa katika vita vikuu vya kwanza vya dunia vilivyodumu kutoka mwaka 1914 hadi mwaka 1918.
Mwaka 1919 sehemu kubwa ya koloni la Kijerumani, ikiwa na wakazi 3,500,000 hivi, ilikabidhiwa rasmi mikononi mwa Uingereza kama eneo lindwa chini yamamlaka ya Shirikisho la Mataifakulingana na kifungo 22 cha mkataba wa Versailles.
Waingereza walihitaji jina jipya kwa ajili ya koloni hilo na tangu Januari 1920wakaamua kuliita "Tanganyika Territory" kwa kutumia jina la ziwa kubwa upande wa mashariki ya eneo. [1]
Uhuru na Muungano
Julius Nyerere akidai uhuru wa Tanganyika mwaka 1961.
Zanzibar ilipata uhuru wake tarehe 10 Desemba1963. Uhuru wa usultani ukadumu muda mdogo tu. Mapinduziya tarehe 12 Januari 1964yakamuondoa Sultani. Mauaji ya familianyingi zenye asili ya Kiarabu yakafuata.
Tarehe 26 Aprili 1964 Tanganyika naZanzibar ziliungana kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hapo kiongozi wa Tanganyika Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alipata kuwa Raiswa kwanza (1964-1985) na kiongozi wamapinduzi ya Zanzibar Abedi Amani Karume akawa Makamu wa Kwanza wa Rais.
Tanzania Telegram Groups, Magroup ya Telegram Tanzania, chini ya Rais wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi (1985-1995) iliruhusu mfumo wa vyama vingi vya siasa Tanzania na kuanza mpango wa kurekebisha uchumi kuendana na masharti ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha Duniani.
Rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa (1995-2005) aliendeleza mfumo wa uchumi wa soko huria ambapo 8mashirika ya umma yanabinafsishwa.
Tarehe 21 Desemba 2005 Jakaya Kikwete aliapishwa kuwa Rais wa nne wa taifa (2005-2015), naye aliendeleza sera za watangulizi wake akitokea chama hichohicho cha CCM.
Don't forget to subscribe In our channel and share this post..
Don't forget to subscribe In our channel and share this post..
Nice man
ReplyDeleteNice
ReplyDelete